

Lugha Nyingine
双子座和什么座最配对
Kenya na Uganda zimetiliana saini hati nyingine nane za maelewano (MoUs) jana Jumatano mjini Nairobi, Kenya, chini ya mikataba 17 ambayo tayari ipo, ili kuimarisha ushirikiano wa kisheria na kitaasisi katika sekta za kimkakati.
Hafla ya utiaji saini huo ilishuhudiwa na Rais Yoweri Museveni wa Uganda aliyezuru nchini humo na mwenzake wa Kenya William Ruto.
Akizungumza na wanahabari Ruto alisema makubaliano hayo ya ushirikiano kati ya Shirika la Taifa la Takwimu la Kenya na Bodi ya Taifa ya Takwimu ya Uganda yametiwa saini ili kuimarisha mabadilishano ya maarifa ya kisayansi na kiufundi.
Kwa upande wake, Museveni alisisitiza kuwa uchumi wa kisasa unachochewa na uzalishaji wa bidhaa na huduma, akihimiza vijana kujikita katika kutumia fursa kubwa ya soko la Afrika.
Ruto na Museveni wameahidi kufanya juhudi za kuimarisha taasisi za kikanda na kuendeleza malengo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ikiwemo kupiga hatua kuelekea umoja wa forodha, soko la pamoja, sarafu moja na shirikisho la kisiasa.
Mandhari ya Kipekee ya Karst katika Mkoa wa Guizhou yavutia watalii
Tamasha la kimataifa la densi lafunguliwa katika Mkoa wa Xinjiang, China likiwa na maonyesho 52
Wakulima wa China wawa na pilikapilika za uzalishaji wa kilimo katika kipindi cha Dashu
Maliasili nyingi za chumvi zaongeza mapato ya wanakijiji katika Wilaya ya Gegye, Xizang, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma